MAMLAKA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI STADI
TAARIFA FUPI YA CHUO CHA VETA IRINGA
CHUO CHA MAFUNZO YA UFUNDI STADI NA HUDUMA IRINGA
Mheshimiwa mgeni rasmi: Mjumbe wa bodi ya VETA Kanda ya Nyanda za juu
Mkurugenzi wa VETA Kanda ya nyanda za juu,
Wakuu wa taasisi mbalimbali,
Waandishi wa habari,
Wageni mbalimbali walio pamoja nasi,
Wafanyakazi wenzangu wote wa VETA
Wahitimu wote,
wanafunzi wote wanaoendelea na mafunzo,
mabibi na mabwana,
Awali ya yote nakushukuru sana wewe binafsi kwa kukubali kushiriki nasi katika Mahafali haya ya 15 ya Chuo chetu.
Aidha niwapongeze kwa dhati kabisa wageni wetu wote kuja kushiriki nasi katika kuwapongeza na hatimaye kuwatunuku Vyeti Wanachuo wetu ambao wamehitimu mafunzo yao.
Mheshimiwa mgeni rasmi,
Chuo cha Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi na Huduma cha Mkoa wa Iringa kinamilikiwa na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi Tanzania (VETA).
Chuo hiki kilifunguliwa rasmi na kuanza utoaji wa Mafunzo mnamo January 1997.
1.Mafunzo yotolewayo
Mheshimiwa mgeni rasmi,
Chuo chetu kinatoa mafunzo ya muda mrefu na mafunzo ya muda mfupi.
· Mafunzo ya muda mrefu yatolewayo hadi sasa ni ya fani mbalimbali kumi na moja (11) kama ifuatavyo:-
1. Umeme wa majumbani
2. Uhazili
3. Useremala
4. Uashi
5. Utengenezaji wa Magari
6. Uungaji vyuma
7. Ukerezaji na Uchongaji Vyuma
8. Upakaji rangi Majengo na Maandishi
9. Ufundi bomba
10. Ushonaji nguo
11. Utayarishaji wa Vyakula
Mafunzo ya muda mfupi
Mheshimiwa mgeni rasmi,
Sambamba na Mafunzo ya muda mrefu Chuo kinatoa pia Mafunzo ya muda mfupi kulingana na mahitaji ya mteja. Zifuatazo ni kozi ambazo Chuo kimeendelea kuzitoa:-
· Udereva
· Kompyuta
· Uhazili
Mheshimiwa Mgeni rasmi,
Chuo kina jumla ya wanafunzi 303 hadi tarehe ya leo (Wasichana 79 Wavulana 224) wasichana asilimia 26.1 Wavulana asilimia 73.9
NA.
FANI
L -I MWAKA WA 1
L-I MWAKA WA 2
L - 2
WAS
WAV
JUML
WAS
WAV
JUMLA
WAS
WAV
JUMLA
JUMLA KUU
1.
USEREMALA
0
09
09
0
16
16
25
2.
UMEME
01
20
21
0
19
19
40
3.
UHAZILI
22
02
24
16
0
16
40
4.
BOMBA
02
13
15
0
07
07
22
5.
UCHONGAJI
V YUMA
01
17
18
0
12
12
30
6.
UUNGAJI VYUMA
01
18
19
0
15
15
34
7.
UASHI
0
08
08
0
15
15
23
8.
UTAYARISHAJI CHAKULA*
16
02
18
-
-
-
-
-
-
18
9.
RANGI NA MAPAMBO
02
11
13
05
08
13
-
-
-
26
10.
USHONAJI NGUO
09
02
11
04
0
04
15
11.
MAGARI
0
18
18
0
12
12
30
JUMLA
42
68
110
33
99
132
04
57
61
303
2.WAHITIMU
Mheshimiwa mgeni rasmi
Katika Mahafali ya leo tunao Vijana 79 (wasichana 20 sawa na asilimia 25.3 na Wavulana 59 sawa na asilimia 74.7
NA.
FANI
WASICHANA
WAVULANA
JUMLA
1.
Uzalishaji Chakula
16
02
18
2
umeme
0
19
19
3
Ushonaji Nguo
04
0
04
4.
Useremala
0
16
16
5.
Bomba
0
07
07
6.
Uashi
0
15
15
Jumla
20
59
79
3. Mafanikio
Mheshimiwa mgeni rasmi,
Katika kutekeleza majukumu yake na malengo mbalimbali Chuo kimepata mafanikio yafuatayo:-
3.1 Kozi fupi
Mwaka huu wa 2011 Chuo kinategemea kutoa jumla ya wahitimu wa kozi fupi zaidi ya 400).
3.2 Kujitangaza
Kwa kutumia vyombo mbalimbali vya habari, Chuo kimekuwa kikiyatangaza mafunzo yake na huduma mbalimbali zinazotolewa hapa,hatimaye kupata mwitikio unaostahili.
3.3 Mafunzo ya Watumishi
Waalimu 05 wamekwenda kuchukua Mafunzo mbalimbali ya muda mrefu. Na Mkutubi 01.
3.4 Huduma mbalimbali:-
Chuo kimeendela kutoa huduma mbalimbali kama
Kantini inavyotoa huduma ya vyakula na vinywaji kwa wateja mbalimbali.
Hostel ya wageni yenye vyumba 20
Kumbi mbalimbali za mikutano na sherehe
3.5 Chuo kimeweza kukamilisha hadi sasa majukumu yake kulingana na mpango kazi.
3.6 Kwa kushirikina na Wanachuo, kazi mbalimbali zilifanyika kwenye karakana, kazi za nje, michezo na shughuli za mazingira zimetekelezwa na zinaendelea kutekelezwa ipasavyo.
3.7 Chuo kimeendelea kushirikina na taasisi mbalimbali ndani na nje ya Iringa katika kuboresha utendaji kazi.
3.8 Mipango yetu mwakani:
Mategemeo ya mwakani ni kupanuwa fani ya utayarishaji wa vyakula kwa kuanzisha idara za
· Front office.
· House keeping.
· Food bevarage and selling.
3.9 Mipango ya baadaye.
Kwa vile eneo la chuo chetu ni Kidogo pengine kuliko vyuo vyote vya VETA Tanzania, chuo kina mpango wa kujenga mabweni eneo la Kitwiru ili kuongeza idadi ya Wanafunzi.
4. Changamoto
Mheshimiwa mgeni rasmi,
Kila penye mafanikio na changamoto zinakuwepo, kwa mfano:-
4.1 Mafunzo kwa vitendo (Field training), ili vijana waweze kuwa mahiri katika fani zao, mafunzo kwa vitendo ni muhimu sana.
Pamoja na jitihada za Chuo za kutafuta sehemu mbalimbali za kufanyia mafunzo hayo: kumekuwepo vikwazo kadhaa kama vile, Wadau wengine kukataa kuwapokea vijana, kwa kudai gharama za mafunzo yao wanapokuwa kwenye sehemu zao.
4.2 Chuo kina uwezo wa kuchukuwa wanafunzi zaidi ya 350 lakini mabweni yaliyopo huchukuwa wanafunzi 106 tu kati ya hao wasichana ni 30 na wavulana ni 76 hivyo kusababisha waombaji wengi kutochukuliwa kujiunga na Chuo.Tumejaribu kutafuta Mabweni ya bei nafuu ndani ya Manispaa ya Iringa lakini tumeshindwa.
4.3 Michezo
Kutokana na eneo la Chuo kuwa dogo, Wanachuo wanapata matatizo ya kushiriki kikamilifu kwenye michezo mbalimbali baada ya masomo.Hata hivyo tunawashukuru jirani zetu wa shule ya Msingi Mlandege ambao wamekuwa wakitusaidia kutatua tatizo hili.
4.4 Maji
Chuo kimekuwa kikikabilina na tatizo la kukatika maji kutoka vyanzo vya JR IRUWASA na hivyo kuathiri mafunzo na utoaji wa huduma nyinginezo za hapa Chuoni.
4.5 Umeme
Chuo kama sehemu ya jamii kimeendelea kupambana na adha ya kukatika mara kwa mara kwa umeme ambao ni nishati muhimu katika kutekeleza majukumu yake kitendo ambacho suluhisho lake ni kuwa na jenereta lenye uwezo mkubwa.
5. Hitimisho
Mheshimiwa mgeni rasmi,
Ninachukua fursa hii, kuwapongeza sana Wanachuo kwa juhudi, usikivu wao na nidhamu katika ufuatiliaji wa mafunzo yao na hivyo kuleta mafanikio makubwa kwao na kwa Chuo chetu.
Tunaowaomba waendelee na ari hiyo ili waweze kuboresha maisha yao huko waendako.
Aidha, tunawaomba wahitimu wetu wawe mabalozi wetu wazuri kuwashauri Vijana wenzao kujiunga na Vyuo mbalimbali vya Mafunzo ya ufundi Stadi, kwani Ufundi ni jibu la haraka katika harakati za kupambana na kutokomeza umaskini hasa pale ambapo kijana ataajiriwa au kujiajiri.
Ahsanteni sana.
URITHI WA KWELI NI ELIMU
Monday, November 28, 2011
Monday, September 13, 2010
BARABARA YA MAFINGA-KIBAO NI BARABARA MBOVU INYOCHANGIA UCHUMI WA TAIFA
Barabara hii ya Kibao -Mafinga ni barabara inayoiwezesha wilaya ya Mufindi mkoani Iringa kuwa mbele katika makusanyo ya mapato na ni moja kati ya barabara zinazochangia kukuu kwa uchumi wa Taifa la Tanzania kutokana na ukubwa wa kiwanda cha karatasi Mgogolo ambacho ni kiwanda kimojawapo kikubwa kwa Afraka ila barabara yake hadi sasa haina hata chembe ya lami
Hii ni
Friday, September 10, 2010
THOMAS SIMON NYIMBO WA CHADEMA AIWEKA PABAYA CCM NJOMBE MAGHARIBI
Thursday, September 2, 2010
FARAJA MAFINGA SACCOs YATOA MISAADA KWA YATIMA 300 MUFINDI
Chama cha ushirika cha kuweka na kukopa cha Faraja Mafinga wilaya ya Mufindi mkoani Iringa kimetoa msaada wa mahitaji mbali mbali kwa watoto yatima zaidi ya 300 wanaosoma katika shule za msingi wilayani Mufindi.
Meneja mkuu wa Faraja Mafinga Clever Ndanzi alizitaja a shule zilizonufaika na msaada huo kuwa ni pamoja na shule ya mzingi Upendo ,Mkombwe zote na mjini Mafinga na shule ya msingi Mtula na Matanana wilizopo nje ya mji wa Mafinga na kuwa kila shule watoto yatima 75 watapatiwa msaada huo.
Aliitaja misaada ilitolewa na Chama hicho kwa yatima hao ambao ni msaada uliotokana na sehemu ya faida ya mapato ya mwaka kwa chama hicho ,kuwa ni pamoja na sababuni,mafuta ya kupakaa na vifaa mbali mbali vya shule .
Kwani amesema kuwa chama hicho kimekuwa na utaratibu wa kutumia faida yake inayopatikana kwa mwaka kwa jaili ya kuisaidia jamii yenye shida mbali mbali wakiwemo yatima na watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi pamoja na waathirika wa janga la Ukimwi ndani ya wilaya hiyo.
Ndazi alisema kuwa ushirikia huo ulianzishwa mwaka 1999 na wanachama 18 ambapo hadi sasa kuna jumla ya wanachama zaidi ya 650 ambapo jumla ya mikopo iliyotolewa hadi sasa kwa wanachama wake ni zaidi ya shilingi bilioni 1.
Kwa upande wake mwenyekiti wa ushirika huo Macelina Mosha alisema kuwa pamoja na kuwasaidia watoto hao bado jamii ya wilaya ya Mufindi inanalojukumu la kuendelea kuwasaidia watoto yatima huku akiahidi kuwa chama chake kitaendelea kuwasaidia watoto hao kutokana na faida inayopatikana kila mwaka.
Bi Mosha alisema kuwa mikakati na mwelekeo wa chama hicho unataraji kufahamika wazi siku ya jumamosi wiki hii wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa wanachama ambapo pia wanachama watapokea taarifa ya mwaka ya chama na kujua makisio na mapato na matumizi ya mwaka 2011.
MWISHO
Meneja mkuu wa Faraja Mafinga Clever Ndanzi alizitaja a shule zilizonufaika na msaada huo kuwa ni pamoja na shule ya mzingi Upendo ,Mkombwe zote na mjini Mafinga na shule ya msingi Mtula na Matanana wilizopo nje ya mji wa Mafinga na kuwa kila shule watoto yatima 75 watapatiwa msaada huo.
Aliitaja misaada ilitolewa na Chama hicho kwa yatima hao ambao ni msaada uliotokana na sehemu ya faida ya mapato ya mwaka kwa chama hicho ,kuwa ni pamoja na sababuni,mafuta ya kupakaa na vifaa mbali mbali vya shule .
Kwani amesema kuwa chama hicho kimekuwa na utaratibu wa kutumia faida yake inayopatikana kwa mwaka kwa jaili ya kuisaidia jamii yenye shida mbali mbali wakiwemo yatima na watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi pamoja na waathirika wa janga la Ukimwi ndani ya wilaya hiyo.
Ndazi alisema kuwa ushirikia huo ulianzishwa mwaka 1999 na wanachama 18 ambapo hadi sasa kuna jumla ya wanachama zaidi ya 650 ambapo jumla ya mikopo iliyotolewa hadi sasa kwa wanachama wake ni zaidi ya shilingi bilioni 1.
Kwa upande wake mwenyekiti wa ushirika huo Macelina Mosha alisema kuwa pamoja na kuwasaidia watoto hao bado jamii ya wilaya ya Mufindi inanalojukumu la kuendelea kuwasaidia watoto yatima huku akiahidi kuwa chama chake kitaendelea kuwasaidia watoto hao kutokana na faida inayopatikana kila mwaka.
Bi Mosha alisema kuwa mikakati na mwelekeo wa chama hicho unataraji kufahamika wazi siku ya jumamosi wiki hii wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa wanachama ambapo pia wanachama watapokea taarifa ya mwaka ya chama na kujua makisio na mapato na matumizi ya mwaka 2011.
MWISHO
Monday, August 30, 2010
MFANYABIASHARA MAARUFU IRINGA AFUNGWA JELA KWA WIZI WA MAHINDI

Mahakama ya hakimu mkazi wa mkoa wa Iringa imemhukumu kifungo cha mwaka moja jela na faini ya shilingi milioni 1 mfanyabiashara maarufu mjini Makambako wilaya ya Njombe mkoani Iringa Bw Mohamed Khalifa Mnyagani kwa kosa la uchepushaji mahindi ya msaada tani 10.pichani ni kamanda wa Takukuru mkoa wa Iringa Bw Donacian Kessy,habari zaidi soma hapa
Wednesday, August 18, 2010
MONICA MBEGA AJITOKEZA KUCHUKUA FOMU YA UBUNGE
Monica Mbega akitoka katika ofisi ya msimamizi mkuu wa uchaguzi jimbo la Iringa kuchukua fomu ya kugombea ubunge jimbo hilo leo
Hapa akiingia katika gari tayari kwa safari ya kurudi ofisi za CCM
Monica Mbega akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuchukua fomu leo na kumpongeza Frederick Mwakalebela kwa kuokoa jahazi kuzama
Msimamizi wa uchaguzi jimbo la Iringa Teresia Mahongo (kushoto) akimkabidhi fomu Monica Mbega
Wapambe wa Mbega wakiwa nje wakisubiri atoke kuchukua fomu .Soma hapa
Monday, August 16, 2010
Subscribe to:
Posts (Atom)