AMANI YETU TUSIIVURUGE WATANZANIA

AMANI  YETU TUSIIVURUGE  WATANZANIA

POLISI JAMII NA ULINZI SHIRIKISHI AMANI NA UTULIVU VITATAWALA DAIMA TANZANIA

Thursday, October 29, 2009

RAIS JAKAYA KIKWETE AMJULIA HALI DIWANI ALIYEKATWA MIGUU IRINGA


Diwani wa kata ya Mseke Iringa Aldo Mwihava ambaye kwa sasa ni mlemavu wa maisha baada ya kukatwa miguu yote akiwa na Rais Jakaya Kikwete nyumbani kwake Mseke jana

Wednesday, October 21, 2009

HOFU YAPUNGUA KWA WANAFUNZI IDODI SEKONDARI


Wanafunzi wa sekondari ya Idodi Iringa wakiendelea na masomo yao kama kawaida ,wanafunzi hao wamelejea katika hali ya utulivu baada ya kumaliza maombolezo ya vifo vya wanafunzi wenzao 12 ambao walikufa kwa moto bwenini agosti 23 mwaka huu

Monday, October 19, 2009

BREAKING NEWSsssssssssssssssss DINI YA AJABU IRINGA YASABABISHA MWANDISHI HUYU KUFARIKI DUNIA..........


Mwandishi Rose Majani wa Radio Country Fm Iringa amefariki dunia kifo chake kimetokana na dini kumzuia kunywa dawa wala kwenda hospitali

Thursday, October 15, 2009

SERIKALI YAMWAGA PONGEZI KWA CHUO CHA TUMAINI IRINGA






Prof.John Shao akizungumza katika uzindunzi wa warsha ya maendeleo ya biashara na ujasiliamali iliyoandaliwa na chuo kikuu kishiriki cha Tumaini Iringa leo










Naibu waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu (TAMISEMI) Aggrey Mwanri (kulia) akimpongeza mratibu wa warsha ya maendeleo ya biashara na ujasiliamali chuo kikuu cha Tumaini Dr Bukaza Chachage leo chuoni hapo










Mkuu wa chuo cha Tumaini Iringa Prof Nicholaus Bangu akiwahotubia wana warsha









Mkuu wa mkoa wa Iringa Mohamed Abdulaziz akimkaribisha mgeni rasimi Naibu waziri wa TAMISEMI











Naibu waziri wa TAMISEMI Aggrey Mwanri (wa nne kushoto) akiwa na viongozi wa chuo kikuu cha Tumaini Iringa pamoja na viongozi wa chama na serikali na washiriki wa warsha hiyo leo


Soma habari hii hapa

Saturday, October 10, 2009

WANAFUNZI WAKWEPA MASOMO WAUZA KUNI.......















Wanafunzi wa shule za msingi Idofi na saja wilaya ya Njombe wakitafuta wateja wa kuni mjini Makambako umbali wa Km zaidi ya 20 kutoka kijijini kwao, kuni ambazo wamekuwa wakiza kwa mzigo sh.500 hadi 800 imeelezwa kuwa idadi ya wanafunzi kukwepa vipindi na kufanya biashara ya kuni imekuwa kubwa katika kata ya saja makambako

Thursday, October 8, 2009

BREAKING NEWSsssssssssssssssss MOTO MWINGINE IDODI SEKONDARI


Huku Taifa likiwa katika maombolezo ya vifo vya wanafunzi 12 wa kike katika shule ya sekondari Idodi waliokufa moto na kuendelea kuuguza majeruhi 23 wa ajali hiyo ya moto baada ya bweni hili kuteketea kwa moto hivi karibuni moto ambao chanzo chake ni mshumaa, wanafunzi wa kiume katika shule hiyo leo wamenusurika kuteketea kwa moto baada ya moto kuibuka ghafla katika moja kati ya mabweni ya muda yanayotumiwa na wavulana hao kwa sasa .

Taarifa za kuaminika zilizothibitishwa na viongozi wa serikali ya kijiji cha Idodi na shule hiyo zinadai kuwa chanzo cha moto huu bado hakijafahamika japo moto huo ulianza kuwaka kutoka ndani ya sa nduku la mwanafunzi mmoja wa kiume bwenini humo .

Hata hivyo moto huo haujaleta maafa yoyote baada ya kuzimwa mapema.

Kwa habari zaidi juu ya tukio hili endelea kutembelea blog hii napenda kukutakia usiku mwema.

Monday, October 5, 2009

SHERIA ZA MIPANGO MIJI IRINGA VINAVYOCHANGIA UBOVU WA MJI


Sheria ngumu ya mipango miji katika Manispaa ya Iringa ambayo imekuwa ikizuia wananchi kufanya matengenezo ya nyumba zao hadi pale wanapoomba kibali cha kujenga nyumba za ghorofa imezidi kuuchakaza mji wa Iringa zaidi ,pichani ni moja ya nyumba ambayo ipo mjini Iringa na bado watu wanaishi ila kuta zake zinataka kuanguka na hivyo kushikiliwa na nguzo na kama sheria hiyo isigekuwepo yawezekana kabisa nyumba hii ingefanyiwa marekebisho

Thursday, October 1, 2009

IDODI SASA NI FURAHA TUPU.........................


Wanafunzi wa shule ya sekondari Idodi Iringa ambao hivi karibuni walikuwa katika msiba mkubwa kwa kupoteza wenzao 12 katika tukio la moto ,wakicheza ngoma jana wakati wakiwaaga wanafunzi wa kidato cha nne shuleni hapo

IDODI SEKONDARI FURAHA TELE LEO..............



Wanafunzi wanaobaki katika shule ya sekondari Idodi wakitoa burudani ya ngoma kwa wa nafunzi wa kidato cha nne wakati wa sherehe za kuwaaga leo


Hii ni familia ya Lukuvi


Hatuamini kama leo tumefikia kikomo hapa Idodi sekondari





Mwalimu Conso Lukuvi akimvisha Levina Lukuvi taji baada ya kuhitimu elimu ya Sekondari Idodi ,wanafunzi hao wanataraji kuanza mitihani yao ya mwisho jumatatu hivyo blog hii inaendelea kuwaombea heri katika mitihani yao,
Usikose kupata makala ya Idodi sekondari katika gazeti la Tanzania daima
Kama unataka kurudi mwanzo bonyeza hapa