AMANI YETU TUSIIVURUGE WATANZANIA

AMANI  YETU TUSIIVURUGE  WATANZANIA

POLISI JAMII NA ULINZI SHIRIKISHI AMANI NA UTULIVU VITATAWALA DAIMA TANZANIA

Thursday, December 24, 2009

RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE AUNGANA NA YATIMA IRINGA KUSHEREKEA KRISMASI...........







SIKU moja baada ya mnajimu maarufu, Barani Afrika, Sheikh Yahya Hussein kubashiri kuwa mtu atakayejitokeza kushindana na Rais Kikwete kwa ajili ya urais awamu ya pili mwakani atakufa ghafla watoto yatima wa kituo cha Tosamanganga Iringa wametuma salama za Krismas na mwaka mpya kwa Rais Kikwete huku wakimwombea mafanikio makubwa katika uchaguzi mkuu mwaka 2010.

Watoto hao zaidi ya 200 waliopo kituoni hapo walituma salama hizo leo mbele ya katibu tawala wa mkoa wa Iringa Getrude Mpaka wakati wakipokea msaada wa chakula kwa ajili ya sikukuu ya Krismas na Mwaka mpya uliotolewa na Rais Kikwete kwa watoto wa kituo hicho.

Katika risala yao iliyosomwa na mkuu wa kituo hicho Sista Helena Kihwele watoto hao walisema kuwa mbali ya kumpongeza Rais Kikwete kwa upendo wao kwao kwa kuwakumbuka kwa chakula hicho ila bado wao wanapenda kutoa zawadi kwake ya maombi zaidi ili kuhakikisha mwaka 2010 unakuwa ni mwaka wa mafanikio makubwa kwake na Taifa zima la Tanzania .

“Mheshimiwa Rais kweli tunashukuru kwa kutukumbuka watoto yatima wa kituo cha Tosamanganga Iringa kwani wapo yatima wengi sana nchini na vituo vipo vingi ila umetuona sisi….tunaamini umeongozwa na Mungu na sisi tunapenda kutoa shukrani zetu kwa salam za heri ya krismasi na mwaka mpya kwa zawadi ulizotoa ….na zawadi yetu kwako ni kuendelea kukuombea mafanikio mema mwaka 2010…tunakupa ahadi ya msaada was ala zetu kwako”

Walisema kuwa wamelazimika kufanya hivyo ili kumwezesha kuwa na afya njema na kutenda shughuli zake kwa Taifa kwa nguvu ya Mungu .

Pamoja na kupongeza na zawadi hiyo ya sikukuu kwa Rais Kikwete pia walisema kituo hicho kinakabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwemo ya vijana wakubwa wanaoruhusiwa kutoka kituoni hapo kurudi kuomba msaada wa elimu kituoni hapo jambo ambalo wanaomba serikali kutoa msaada kwa vijana hao wa kielimu na miradi ya kimaendeleo zaidi.

Kituo hicho kina jumla ya watoto 479 huku watoto 253 wanaishi kituoni hapo na watoto 226 wanapewa misaada wakiwa majumbani kwao.

Akikabidhi msaada huo kwa niaba ya Rais Kikwete katibu tawala wa mkoa wa Iringa Mpaka alisema kuwa Rais amewatakia watoto hao fanaka kwa Krismasi na mwaka mpya wa 2010 .

Alisema kuwa Rais amefarijika sana kushiriki na watoto hao katika kusherekea sikukuu hizo mbili ikiwemo ya Krismasi ambayo inasherekewa kesho kote duniani na ile ya Mwaka mpya na kuwa kwa upande wake alipenda kufika kula na watoto hao kama njia ya kudumisha upendo kwao

Hata hivyo kutokana na sababu zisizo zuilika amelazimika kutoa zawadi ya chakula chenye thamani ya zaidi ya shilingi 607,000 kwa ajili ya kuungana na watoto hao katika sikukuu ya Krismasi na mwaka mpya.

Mmiliki wa Blog hii anapenda kuungana na wakristo wote ulimwenguni katika kusherekea sikuu ya Krismasi na Mwaka mpya pia kwa watanzania tuige mfano wa Rais Kikwete kula na Yatima

RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE AUNGANA NA YATIMA IRINGA KUSHEREKEA KRISMASI...........









Na Francis Godwin,Iringa

SIKU moja baada ya mnajimu maarufu, Barani Afrika, Sheikh Yahya Hussein kubashiri kuwa mtu atakayejitokeza kushindana na Rais Kikwete kwa ajili ya urais awamu ya pili mwakani atakufa ghafla watoto yatima wa kituo cha Tosamanganga Iringa wametuma salama za Krismas na mwaka mpya kwa Rais Kikwete huku wakimwombea mafanikio makubwa katika uchaguzi mkuu mwaka 2010.

Watoto hao zaidi ya 200 waliopo kituoni hapo walituma salama hizo leo mbele ya katibu tawala wa mkoa wa Iringa Getrude Mpaka wakati wakipokea msaada wa chakula kwa ajili ya sikukuu ya Krismas na Mwaka mpya uliotolewa na Rais Kikwete kwa watoto wa kituo hicho.

Katika risala yao iliyosomwa na mkuu wa kituo hicho Sista Helena Kihwele watoto hao walisema kuwa mbali ya kumpongeza Rais Kikwete kwa upendo wao kwao kwa kuwakumbuka kwa chakula hicho ila bado wao wanapenda kutoa zawadi kwake ya maombi zaidi ili kuhakikisha mwaka 2010 unakuwa ni mwaka wa mafanikio makubwa kwake na Taifa zima la Tanzania .

“Mheshimiwa Rais kweli tunashukuru kwa kutukumbuka watoto yatima wa kituo cha Tosamanganga Iringa kwani wapo yatima wengi sana nchini na vituo vipo vingi ila umetuona sisi….tunaamini umeongozwa na Mungu na sisi tunapenda kutoa shukrani zetu kwa salam za heri ya krismasi na mwaka mpya kwa zawadi ulizotoa ….na zawadi yetu kwako ni kuendelea kukuombea mafanikio mema mwaka 2010…tunakupa ahadi ya msaada was ala zetu kwako”

Walisema kuwa wamelazimika kufanya hivyo ili kumwezesha kuwa na afya njema na kutenda shughuli zake kwa Taifa kwa nguvu ya Mungu .

Pamoja na kupongeza na zawadi hiyo ya sikukuu kwa Rais Kikwete pia walisema kituo hicho kinakabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwemo ya vijana wakubwa wanaoruhusiwa kutoka kituoni hapo kurudi kuomba msaada wa elimu kituoni hapo jambo ambalo wanaomba serikali kutoa msaada kwa vijana hao wa kielimu na miradi ya kimaendeleo zaidi.

Kituo hicho kina jumla ya watoto 479 huku watoto 253 wanaishi kituoni hapo na watoto 226 wanapewa misaada wakiwa majumbani kwao.

Akikabidhi msaada huo kwa niaba ya Rais Kikwete katibu tawala wa mkoa wa Iringa Mpaka alisema kuwa Rais amewatakia watoto hao fanaka kwa Krismasi na mwaka mpya wa 2010 .

Alisema kuwa Rais amefarijika sana kushiriki na watoto hao katika kusherekea sikukuu hizo mbili ikiwemo ya Krismasi ambayo inasherekewa kesho kote duniani na ile ya Mwaka mpya na kuwa kwa upande wake alipenda kufika kula na watoto hao kama njia ya kudumisha upendo kwao

Hata hivyo kutokana na sababu zisizo zuilika amelazimika kutoa zawadi ya chakula chenye thamani ya zaidi ya shilingi 607,000 kwa ajili ya kuungana na watoto hao katika sikukuu ya Krismasi na mwaka mpya.
MWISHO

Sunday, December 13, 2009

MKE WA MKURUGENZI MAELEZO ATOA ZAWADI ZA KRISMASS KWA YATIMA IRINGA.............











Mke wa mkurugenzi wa Idara ya habari na maelezo Bi Esther Mshana (kulia) akimkabidhi mkurugenzi wa kituo cha yatima cha Daily Bread Life akimkabidhi msaada kwa ajili ya Yatima mkurugenzi wa kituo hicho mchungaji Mpeli Mwaisumbe










Bw Frank Mwaisumbe (kushoto) mchungaji Mpeli Mwaisumbe wakiwa katika picha ya familia leo










Kweli leo mambo yamefana kweli kweli



















Nimefurahi sana ila ndoto zangu bado ni ubunge tu ipo siku nitasema










Ubatizo unaendelea








Kwa makala ya na habari za sherehe hizi usikose kusoma gazeti la Msemakweli jumapili na gazeti la Tanzania daima ama sikiliza wapo radio kesho asubuhi Bonyeza hapa

Saturday, December 12, 2009

MKWAWA NA RUCO WAFANYA MAHAFALI LEO












wahitimu wa chuo cha Ruaha Iringa









Mambo ya mahafali ya pili Chuo kikuu kishiriki cha Ruaha Iringa










Tumependeza kwa mavazi na kiwango cha elimu sasa sisi ni wasomi










Happiness,Belinda na Elizabeth sisi ni wasomi sasa









kazi kubwa ni kulitumikia Taifa katika taaluma yetu ya sheria









Peter akiwa na dadake Violet mara baada ya kutunukiwa shahada ya elimu ya jamii na ualimu katika chuo kikuu cha MKWAWA Iringa









Furaha ya elimu ni kuitumia vyema









Furaha ya wazazi









Lazima leo tupate kumbukumbu za kutosha









Tulia dada nikutengeneze taji









Wakuu wa chuo kikuu cha Elimu Mkwawa









Wimbo wa Taifa heshima kwa Taifa letu









Wahitimu wa chuo kikuu cha elimu Mkwawa wakiwa wametunukiwa vyeti vyao leo


Picha zaidi tembelea mtandao wa www.matukiodaima.blogspot.com leo saa 2 usiku

Friday, December 11, 2009

MATOKEO DARASA LA SABA SOUTHERN HIGHLANDs MAFINGA YATIKISA















Afisa elimu mkoa wa Iringa Salum Maduhu akitangaza matokeo ya darasa la saba leo










Afisa elimu taalum mkoa wa Iringa Leonard Msigwa akitoa hali halisi ya mtokeo kati ya mwaka jana na mwaka huu ambapo mkoa wa Iringa umeshuka

Na Francis Godwin,Njombe

MAAJABU ya matokeo ya mtihani wa Taifa wa darasa la saba mwaka 2009 ,shule ya binafsi ya Southern Highlands Mafinga peke yake imeweza wavulana 9 kati ya wavulana 10 bora na kuwa shule ya kwanza kimkoa kati ya shule 830 huku shule 10 za mwisho ni zile zinazo milikiwa na serikali.

Pia maajabu mengine ya matokeo hayo ya darasa la saba mkoani Iringa ni pamoja na mtahiniwa wa MEMKWA Rashid Mdesa kutoka halamsahauri ya wilaya ya Njombe ambaye amefaulu kwa kupata alama 214 na kuchaguliwa kujiunga na shule ya sekondari ya Kibaha .

Shule hiyo ya Southern Highlands Mafinga ni shule inayomilikiwa na afisa elimu (mstaafu) wa wilaya ya Mufindi Mary Mungai na ni moja kati ya shule zinazomilikiwa za binafsi zinazomilikiwa na wanawake hapa nchini.

Akitangaza matokeo hayo leo katika ukumbi wa Nazareth Njombe mbele ya waandishi wa habari na wajumbe wa kamati ya uchaguzi mkoa ,afisa elimu mkoa wa Iringa Salum Maduhu alisema kuwa kwa mwaka huu mkoa hautakuwa na uchaguzi wa pili wa wanafunzi na kuwa kati ya weanafunzi 50,604 aliofanya mtihani huo mwaka huu kati yao wanafunzi 30,187 sawa na asilimia 59.65 wamefaulu mtihani huo na kuchanguliwa kwa ajili ya kuanza masomo ya sekondari mwakani 2010.

Hata hivyo alisema kuwa pamoja na mkoa wa Iringa kuendelea kujivunia kwa kushikilia nafasi ya tatu kitaifa kwa miaka mitatu mfululizo sasa bado hali ya matokeo kwa mwaka huu yanaonyesha kushuka kwa kiwango cha asilimia 4.43 kuwa wilaya zote zimeshuka ukilinganisha na mwaka 2008.

Kwani alisema mwaka 2008 watahiniwa walifaulu mtihani huo walikuwa 34,528 sawa na asilimia 64.01 hivyo ukilinganisha na maka huu hali imeshuka kiasi.

Akitangaza majina ya wanafunzi wavulana 10 bora kimkoa na shule walizotoka katika mabano alisema kuwa mwanafunzi Jared Kinzila aliyepata alama 226 (Southern Highlands ) atakwenda shule ya Iboru,Hildigard Mawondo alama 222(Southern Highlands atajiunga na shule ya sekondari ya Iyunga,Gift Nnko alama 221(southern Highlands) atajiunga na sekondari ya Kibaha,Honest Mwakabungu alama 220 amechaguliwa kujiunga na sekondari ya Kantalamba,Joshua Ngailo alama 220 (southern Highalnds ) atakwenda Moshi Tech na Grant Kilongo alama 220 (St.Benedict Njombe) amechanguliwa kujiunga na Ilboru.

Wengine ni Laban Makila aliyepata alama 219 (southern Highalnds) amepangiwa Ifunda,Mika Lwila aliyepata alama 219(southern Highalnds ) atakwenda kibaha,Ben Msigala aliyepata alama 218 (southern Highlands ) atakwenda JJ.Mungai na Fredrick Urio aliyepata alama 218 (southern Highalnd ) aliyechaguliwa kujiunga na sekondari ya kilosa.

Kwa upande wa wasichana kumi bora aliyeongoza na Doris Ndamugoba aliyepata alama 220 (St .Benedict ) aliyechaguliwa kujiunga na sekondari ya Kilakala,Beatrice Mwaitete alama 218(St Benedict) atakayejiunga na sekondari ya Msalato,Edna Mwakeja aliyepata alama 216(Nyumbatatu Iringa) atakaye kwenda Kilakala,Doreen Malavanu aliyepata alama 216 ( Brooke Bond) shule aliyopangiwa ni Kilakala,Lucy Luoga alama 216(Amani Ludewa) kwenda Kilakala, na Hawa Mpakate alama 215 ( Southern Highlands).

Wengine ni Amaria Mramba alama 215(St.Benedict ) kwenda Iringa Girls,Clara kalimwenjuma alama 215(St Benedict) Mtwara ufundi,Given Mndewa alama 214(St Benedict) Mabatini na Agatha Luoga alama 214(Amani Ludewa) Msalato.

Alizitaja shule kumi zilizofanya vibaya na nafasi iliyoshika katika mabano ya mwisho ni Idunda Kilolo ( 830) kati ya shule 830 za mkoa wa Iringa,Itonya –Kilolo( 829), Mboliboli –Iringa (828),Idasi –Kilolo (827),Mhanga –Kilolo(826),Ilambo –Kilolo( 825),Liugai –Ludewa (824),Mapera Mengi –Iringa(823),Mpanga Tazara –Iringa (822) na Makuka –Iringa (821).

Wakati shule 10 bora na wilaya yake katika mabano shule ya kwanza ni Southern Highlands Mafinda (Mufindi), Livingstone(Njombe),Brooke Bond (Mufindi),St.Benedict(Njombe mji),Star (Manispaa ya Iringa),Kitulo (Makete),Mwera (Makete),Ramadhani (Njombe) St.Dominic Savio (Manispaa ya Iringa shule ya kumi ni Amani (Njombe mji ).

Hata hivyo afisa elimu huyo mkoa aliwataka wazazi wote ambao watoto wao wamechanguliwa kujiunga na elimu ya sekondari mwakani kuanza maandalizi ili mwakani 2010 wote waanze masomo.

“lazima wazazi wajipange kuhakikisha watoto wote wanaanza masomo… mbele kuna sikukuu ya xmass na mwaka mpya ni vyema wazazi kupunguza matumizi makubwa ya sherehe hizo na kutenga ada za watoto “

bofya hapa

Thursday, December 10, 2009

MATOKEO DARASA LA SABU KUTANGANZWA DESEMBA 12


Wanafunzi wa moja kati ya shule ya msingi mkoani Iringa wakiwa chini ya mti wakisubiri mwalimu kwa ajili ya kuwafundisha ,kumbuka kesho ijumaa matokeo ya darasa la saba yatatangazwa nchini

Wednesday, December 9, 2009

BREAKINGNEWzzzzzzzzzzzzzzzzAJALI YAUA WATATU IRINGA






Aliyekuwa dereva wa gari aina ya Tax yenye namba za usajili T 501 APX Bw Juma Jabiri mkazi wa jijini Dar es Salaam akiwa hajitambui katika hospitali teule ya wilaya ya Kilolo (Ilula ) Iringa akipatiwa matibabu baada ya kuokolewa kutoka eneo la tukio ,katika gari leke watu wawili walikufa papo hapo baada ya kugongana na basi la Sumry na gari jingine(picha na Francis Godwin)












Basi la kampuni ya Sumry High Class lenye namba za usajili T 586 AVR Nissan likiwa linaning'inia hewani katika milima ya Kitonga barabara kuu ya Iringa -Dar es Salaam baada ya kugongana na magari mengine madogo mawili ,katika ajali hiyo kwenye basi hakuna mtu aliyepoteza maisha ila katika gari dogo watu wawili walikufa papo hapo (picha na Francis Godwin)


Wakazi wa eneo la Kitonga Iringa wakiangalia Tax yenye namba za usajili T 501 APX ikiwa imeharibika vibaya baada ya kugongana uso kwa uso na basi la Sumry leo mchana watu wawili waliokuwemo katika gari hii walikufa papo hapo(picha na Francis Godwin)
Rudi mwanzo hapa

Thursday, December 3, 2009

SOUTHERN HIGHLANDS SCHOOL NI SHULE YA MSINGI YENYE MCHEPUO WA KIINGEREZA

SOUTHERN HIGHLANDS SCHOOL
(SHS)
SHULE YA MSINGI
YENYE MCHEPUO WA KIINGEREZA
S.L.P 34, MAFINGA, TANZANIA
SIMU NA. 026-2772661
Fax: 026-2772544

Mwalimu Mkuu: 0754 048848

Mkurugenzi Mtendaji: 0754-651966

EMAIL:southernhighlands97@yahoo.com