WAJUMBE wa baraza la ushauri ya mkoa (RCC) mkoani Iringa washindwa kuridhia mapendekezo mapya ya majimbo ya uchaguzi yaliyopendekezwa na halmashauri za wilaya baada ya kukosa sifa zilizotolewa na tume ya uchaguzi ili jimbo liweze kugawanywa.
Pamoja na kuonyesha kuyatosa mapendekezo hayo ya halmashauri bado wilaya ya Njombe kuna uwezekano wa kupata jimbo jipya katika mji wa Makambako baada ya wilaya hiyo kuwa na mchakato wa kuubariki mji wa Makambako kuwa mji rasmi wajumbe wameridhia hilo.
Wakijadili katika kikao cha dharula baraza la uhauri la mkoa (RCC) leo kilichofanyika katika ukumbi wa Siasa ni kilimo chini ya mwenyekiti wake mkuu wa mkoa wa Iringa Mohamed Abdulaziz .
Wajumbe hao walishindwa kutetea hoja ya kwanini majimbo ya uchaguzi yaongezwe katika wilaya zao pamoja na kukosa sifa za tume zilizotolewa kwa mikoa yote hapa nchini baada ya baadhi ya mikoa kuwepo kwa taarifa ya kuchukua kazi ya tume ya uchaguzi kwa kujitangazia mapya kinyume na utaratibu.
Mbunge wa jimbo la Njombe Kaskazin Mzee Jackson Makwete na mbunge wa jimbo la Kilolo Prof.Peter Msolla ndio wabunge pekee waliofika katika kikao hicho nyeti kati ya wabunge 13 wa majimbo 11 na wawili wa viti maalum mkoa wa Iringa.
Akichangia hoja ya kuongeza majimbo katika wilaya ya Njombe mbunge Makwete alisema kuwa ni vyema busara zikatumika katika kujadili suala hilo ili wilaya ya Njombe ikubaliwe kuongezewa jimbo moja zaidi ombi ambalo liliungwa mkono kwa kukubali mji wa Makambako kupendekezwa kuwa jimbo .
Mwenyekiti wa kikao hicho mkuu wa mkoa wa Iringa ambaye ni mbunge wa jimbo la Lindi mjini aliwataka wajumbe kupiga kura wanaotaka Makambako kuwa jimbo na wale wanaopinga pendekezo hilo ambapo wajumbe wote waliunga mkono baada ya kuwepo kwa hoja hiyo nyeti mbele ya Makambako kuwa mji.
Awali wilaya zaidi ya tatu ndani ya mkoa wa Iringa zilikuwa katika mchakato wa kupendekeza ongezeko la majimbo ya uchaguzi kwa madai ya ukubwa wa majimbo hayo na hali ya kijografia katika wilaya sababu ambayo haijaweza kuendana na sifa za tume .
Wilaya zilizokuwa katika mchakato wa mapendekezo ya majimbo mapya ni pamoja na Makete yenye jimbo moja ilipendekezwa kuwe na majimbo mawili ,Njombe yenye Majimbo tatu ilipendekezwa kuwe na majimbo manne ,Ludewa yenye jimbo moja ilitaka kuongeza jimbo la pili na kama Kilolo huku wilaya ya Mufindi ilikuwa ikitaka kuongeza jimbo la tatu kutoka majimbo mawili ya sasa.
Moja ya sifa kubwa iliyokwamisha halmashauri kukosa sifa za kupitishiwa mapendekezo yake ya kugawa majimbo ya uchaguzi ni ile ya idadi ya watu ambapo tume inataka ili jimbo liweze kuwa jimbo lazima liwe na idadi ya watu zaidi ya 200,000 jambo ambalo kwa halmahauri hizo hazijaweza kufikisha zaidi ya kuwa nusu ya idadi hiyo pamoja na sababu nyingine nyingi ambazo zimo katika barua ya tume kwa mikoa yote.
Kabla ya tume kupiga marufuku zoezi la mikoa kutangaza majimbo ya uchaguzi katika mkoa wa Iringa baadhi ya makanda wa CCM wanaotaka kuwania ubunge katika majimbo mbali mbali walianza kujitangazia kuwa wanakusudia kugombea katika majimbo mapya ambayo hata hivyo tume ilikuwa haijataganza zaidi ya kuwepo kwa mapendekezo katika halmashauri pekee.
