AMANI YETU TUSIIVURUGE WATANZANIA

AMANI  YETU TUSIIVURUGE  WATANZANIA

POLISI JAMII NA ULINZI SHIRIKISHI AMANI NA UTULIVU VITATAWALA DAIMA TANZANIA

Saturday, March 27, 2010

MASHINDANO YA VODA COM MUFINDI MUUNGANO CUP 2010 YAZIDI KUNOGA

Mkurugenzi na Voda Com mikoa ya kusini Jackson Kiswaga ( kushoto) akiwa ameshika jezi na mfano ya waziri wa nchi ofisi ya waziri kiongozi (SMZ) Hamza Hassan Juma


TIMU zazidi kukamiana kuwania zawadi ya shilingi milioni 5 ya Voda Com katika mashindano ya kombe la Muungano Mufindi ambayo yamezidi kuwa na msisimko mkubwa na kupelekea timu zilizokuwa zikipewa nafasi kubwa ya kushinda kama wenyeji Igowole na Silver Star na Donbosco kubanwa mbavu na kutolewa katika mashindano hayo .

Huku timu ya benki ya wananchi Mufindi (MuCoba) na watani wao wa jadi timu ya Nyamalala sekondari zote za mjini Mafinga kucheza mchezo wa marudiano kesho jumatatu ili kupata mshindi baada ya kugongana matokeo.

Mratibu wa kombe la Muungano Mufindi Daud Yassin ameueleza mtandao huu kuwa mashindano hayo kwa mwaka huu yamekuwa na msisimko mkubwa ukilinganisha na miaka yote iliyopita kutokana timu kucheza kwa kujituma na nidhamu ya hali ya juu kama njia ya kuwania ubingwa huo wa Voda Com Muungano Cup 2010 ambapo mshindi ataibuka na kombe pamoja na fedha taslimu shilingi milioni 5 tofauti na mwaka jana ambapo mshindi alizawadiwa kombe na shilingi milioni 3 toka Voda com.

Aidha Yassin alisema hali ya mashabiki katika wiwanja kwa mwaka huu imekuwa ya kuvutia na kuwa kila mchezo unapochezwa iwe kituo cha Igowole ama shule ya Msingi Wambi mjini Mafinga wananchi wamekuwa wakiacha shughuli zao na kufika katika viwanja hivyo.


Yassin alisema katika mashindano hayo ambapo timu 10 zinashiriki kwa upande wa bara kutoka mkoa wa Mbeya,Rukwa,Ruvuma na Iringa timu za mkoa wa Iringa ambazo zilianza mashindano hayo jumamosi iliyopita baada ya kufunguliwa na waziri wa nchi ofisi ya waziri kiongozi (SMZ) Hamza Hasan Juma katika viwanja wa shule ya msingi Igowole ,timu hizo zimeendelea kufanya vizuri na zile zilizoshindwa zimeaga mashindano hayo.

Akielezea matokeo toka mwanzo wa mashindano hayo alisema kuwa katika mchezo wa ufunguzi Mucoba na Nyamalala zilitoka suluhu ya bila kufungana huku Don Bosco ikiiadhibu Igowole kwa jumla ya goli 2-1.

Wakati mchezo uliofuata MUcoba iliichapa Silver ya mjini Iringa goli 2-0 sanjari na Nyamalala sekondari iliyoifunga timu hiyo ya Silver Stars 2-0 huku Igowole ikiifunga Kitwiru stars 2-1

Mratibu huyo alisema kuwa hadi sasa michezo sita imemalizika huku Nyamalala Sekondari na Mucoba zitacheza mchezo wa marudiano ili kumpata mshindi baada ya kulingana pointi na magoli

Hata hivyo alisema mara baada ya kupata mshindi wa kituo cha Igowole na Mafinga zoezi litakalofuata ni mchezo wa kumpata bingwa wa jumla katika kituo cha Igowole na Mafinga kabla ya kumtafuta bingwa wa jumla upande wa Tanzania bara atakayecheza na bingwa wa Visiwani.

Hata hivyo alisema ufunguzi wa kituo cha Mbarali Mbeya unataraji kufanyia mwanzo mwa mwezi ujao katika viwanja wa Chimala Mbeya .
MWISHO

Sunday, March 21, 2010

VODA COM YAONGEZA DAU MUFINDI CUP 2010







BINGWA wa jumla wa mashindano ya kombe la Muungano Mufindi upande wa Zanzibar na Bara kuzawadiwa kombe na kitita cha shilingi milioni 5 kutoka kwa wadhamini wakuu wa mashindano hayo Voda Com Tanzania .

Kampuni hiyo ya simu za viganjani Voda Com Tanzania imesema kuwa o kwa mwaka huu imeongeza zawadi kutoka milioni 3 mwaka jana hadi kiasi cha shilingi milioni 5

Voda com imeongeza kiwango hicho cha zawadi kwa lengo la kuboresha zaidi hadhi ya mashindano hayo kwa mwaka huu ambayo yamezinduliwa na waziri wa nchi ofisi ya waziri kiongozi wa serikali ya mapinduzi Zanzibar Hamza Hassan Juma.


Pamoja na Voda Com kuongeza nguvu za udhamini wake katika mashindano hayo mwaka huu kampuni ya Chai bora Mufindi nao wamekuwa miongoni mwa wadau wa soka wilaya ya Mufindi waliovutiwa na jitihada za Voda Com katika mashindano hayo kwa kushiriki kuchangia sehemu ya gharama za udhamini .

Mkurugenzi wa Voda coma nyanda za juu kusini Jackson Kiswaga alisema akikabidhi vifaa vya michezo na mazoezi kwa timu zote zitakazo shiriki katika mashindano hayo mwaka huu alisema kuwa udhamini Voda Com kwa mwaka huu ni kiasi cha shilingi milioni 74 ukilinganisha na mwaka jana ambapo Voda Com ilidhamini mashindano hayo kwa kiasi cha shilingi miliioni 45.

Alisema kuwa udhamini huo ni pamoja na vifaa vya michezo ,zawadi mbali mbali pamoja na mambo mengine katika mashindano hayo isipo kuwa posho kwa viongozi wa timu shilingi.

Hata hivyo alisema kuwa zawadi ya mwaka huu mshindi wa kwanza atanyakua kitita cha shilingi milioni 5 pamoja na kikombe ,mshindi wa pili shilingi milioni 3 na mchezaji bora shilingi 300,000 huku mwamuzi bora atazawadiwa shilingi 300,000.

Pia alisema Voda com watalipia gharama za usafiri malazi pamoja na chakula kwa timu zote zinazotoka nje ya wilaya ya Mufindi .

Kiswaga alisema kuwa kwa upande wa Chai bora wao wameunga mkono jitihada za Voda kwa kudhamini upande wa matangazo katika mashindano hayo .

Hivyo aliwaomba wadau wengine wa michezo kuendelea kujitokeza kudhamini mashindano hayo ambayo yamekuwa yakiendelea kutoa msisimuko mkubwa wa michezo katika mikoa ya kusini hasa mkoani Iringa.

Kwa upande wake mwenyekiti wa mashindano hayo mbunge wa jimbo la Mufindi kusini Benito Malangalila akimkaribisha mgeni rasimi kufungua mashindano hayo ,alisema kuwa mafanikio ya mashindano hayo yametokana na ushirikiano mkubwa uliopo kati ta mratibu wa mashindano hayo Daud Yasin na kamati ya mashindano.

Hata hivyo alisema kuwa toka kuanzishwa kwa mashindano hayo zaidi ya miaka mitano sasa wilaya ya Mufindi imeendelea kupata mafanikio makubwa katika michezo na kuwa moja kati ya wilaya zinazodumisha muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Kwa upande wake waziri Juma pamoja na kumpongeza mratibu wa kombe hilo Yassin na wadhamini wa mashindano hayo Voda Com na Chai Bora pia aliwapongeza wasisi wa mashimndano hayo mbunge wa jimbo la Mufindi Kaskazin Joseph Mungai na mbunge wa jimbo la Mufindi kusini Malangalila.

Pia alisema kuwa ili kuendelea kudumisha Muungano nin vyema timu kuendelea kucheza kwa kujituma zaidi bila kuyageuza mashindano hayo kuwa sehemu ya vurugu na ubaguzi.

Alisema kuwa mashindano hayo ni mashindano makubwa ambayo yanapaswa kupewa heshima kubwa kama ambavyo viongozi wa kitaifa ambavyo wamekuwa wakiheshimu mashindano hayo kwa kufika kufunga na kufungua mashindano hayo.

Katika uzinduzi wa mashindano hayo uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Igowole ,timu ya Benki ya wananchi Mufindi (Mucoba)zilishindwa kufungana na timu ya watani wao wa jadi Nyamalala Sekondari huku mchezo wa pili kati ya wenyeji Igowole Sekondari na Don Bosco ya Iringa ,Igowole ilishindwa kutamba katika uwanja huo wa nyumbani baada ya kukubali kipigo cha goli 2 kwa moja kutoka kwa wageni Don Bosco .

MWISHO
Na Francis Godwin,Mufindi

WADHAMINI wakuu wa mashindano ya kombe la Muungano Mufindi kampuni ya simu za viganjani Voda Com Tanzania wamesema kuwa bingwa wa kombe hilo kwa mwaka huu ameongezewa zawadi kutoka milioni 3 mwaka jana hadi kiasi cha shilingi milioni 5

Voda com imeongeza kiwango hicho cha zawadi kwa lengo la kuboresha zaidi hadhi ya mashindano hayo kwa mwaka huu ambayo yamezinduliwa juzi na waziri wa nchi ofisi ya waziri kiongozi wa serikali ya mapinduzi Zanzibar Hamza Hassan Juma.


Pamoja na Voda Com kuongeza nguvu za udhamini wake katika mashindano hayo mwaka huu kampuni ya Chai bora Mufindi nao wamekuwa miongoni mwa wadau wa soka wilaya ya Mufindi waliovutiwa na jitihada za Voda Com katika mashindano hayo kwa kushiriki kuchangia sehemu ya gharama za udhamini .

Mkurugenzi wa Voda coma nyanda za juu kusini Jackson Kiswaga alisema akikabidhi vifaa vya michezo na mazoezi kwa timu zote zitakazo shiriki katika mashindano hayo mwaka huu alisema kuwa udhamini Voda Com kwa mwaka huu ni kiasi cha shilingi milioni 74 ukilinganisha na mwaka jana ambapo Voda Com ilidhamini mashindano hayo kwa kiasi cha shilingi miliioni 45.

Alisema kuwa udhamini huo ni pamoja na vifaa vya michezo ,zawadi mbali mbali pamoja na mambo mengine katika mashindano hayo isipo kuwa posho kwa viongozi wa timu shilingi.

Hata hivyo alisema kuwa zawadi ya mwaka huu mshindi wa kwanza atanyakua kitita cha shilingi milioni 5 pamoja na kikombe ,mshindi wa pili shilingi milioni 3 na mchezaji bora shilingi 300,000 huku mwamuzi bora atazawadiwa shilingi 300,000.

Pia alisema Voda com watalipia gharama za usafiri malazi pamoja na chakula kwa timu zote zinazotoka nje ya wilaya ya Mufindi .

Kiswaga alisema kuwa kwa upande wa Chai bora wao wameunga mkono jitihada za Voda kwa kudhamini upande wa matangazo katika mashindano hayo .

Hivyo aliwaomba wadau wengine wa michezo kuendelea kujitokeza kudhamini mashindano hayo ambayo yamekuwa yakiendelea kutoa msisimuko mkubwa wa michezo katika mikoa ya kusini hasa mkoani Iringa.

Kwa upande wake mwenyekiti wa mashindano hayo mbunge wa jimbo la Mufindi kusini Benito Malangalila akimkaribisha mgeni rasimi kufungua mashindano hayo ,alisema kuwa mafanikio ya mashindano hayo yametokana na ushirikiano mkubwa uliopo kati ta mratibu wa mashindano hayo Daud Yasin na kamati ya mashindano.

Hata hivyo alisema kuwa toka kuanzishwa kwa mashindano hayo zaidi ya miaka mitano sasa wilaya ya Mufindi imeendelea kupata mafanikio makubwa katika michezo na kuwa moja kati ya wilaya zinazodumisha muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Kwa upande wake waziri Juma pamoja na kumpongeza mratibu wa kombe hilo Yassin na wadhamini wa mashindano hayo Voda Com na Chai Bora pia aliwapongeza wasisi wa mashimndano hayo mbunge wa jimbo la Mufindi Kaskazin Joseph Mungai na mbunge wa jimbo la Mufindi kusini Malangalila.

Pia alisema kuwa ili kuendelea kudumisha Muungano nin vyema timu kuendelea kucheza kwa kujituma zaidi bila kuyageuza mashindano hayo kuwa sehemu ya vurugu na ubaguzi.

Alisema kuwa mashindano hayo ni mashindano makubwa ambayo yanapaswa kupewa heshima kubwa kama ambavyo viongozi wa kitaifa ambavyo wamekuwa wakiheshimu mashindano hayo kwa kufika kufunga na kufungua mashindano hayo.

Katika uzinduzi wa mashindano hayo uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Igowole ,timu ya Benki ya wananchi Mufindi (Mucoba)zilishindwa kufungana na timu ya watani wao wa jadi Nyamalala Sekondari huku mchezo wa pili kati ya wenyeji Igowole Sekondari na Don Bosco ya Iringa ,Igowole ilishindwa kutamba katika uwanja huo wa nyumbani baada ya kukubali kipigo cha goli 2 kwa moja kutoka kwa wageni Don Bosco .


videoVIDEO YA MKURUGENZI WA VODA COM NYANDA ZA JUU KUSINI BW.JACKSON KISWAGA

Thursday, March 11, 2010

MKUU WA AGEUKA MBOGO KWA WANAHABARI IRINGA....................


SIKU moja baada ya wanahabari mkoani Iringa kutishia kumsusia mkuu wa mkoa wa Iringa Mohamed Abdulaziz katika ziara zake ndani ya mkoa kutokana na kupinga ubaguzi wa vyombo vya habari unaofanywa na ofisi yake ,mkuu huyo wa mkoa leo amekutana na wanahabari wa vyombo vyote na kutoa msimamo wa ofisi yake juu ya hatua hiyo ya wanahabari hao kutaka kumsusia na kuwa suala hilo atalitazama kwa kina ili kuondoa tofauti hizo.

Katika kikao chake hicho na wanahabari kilichofanyikia ukumbi wa katibu tawala wa mkoa wa Iringa majira ya saa 4 asubuhi ,pamoja na mambo mengine mkuu huyo alipatwa wakati mgumu kuwajibu wanahabari hao juu ya sababu kutomfikisha makamu wa Rais Dr.Ally Mohamed Shein katika wilaya ya Makete ambayo wanawanchi wake walikuwa na shauku kubwa ya kutembelewa na kiongozi wa kitaifa wakati huu wa masiki ili kushuhudia ubovu wa miundo mbinu katika barabara za wilaya hiyo.

Akitoa ufafanuzi huo huku akiwa ametawaliwa na jazba kubwa kwa baadhi ya vyombo visivyo wa serikali kuwa vimekuwa vikiandika mabaya pekee yanayojitokeza na kuacha mambo mengi mazuri ,alisema kuwa sababu ya wanahabari wachache kutumika katika ziara hizo za viongozi wa kitaifa linasababishwa na wahariri wa vyombo husika ambao wamekuwa wakipanga waandishi wao kutoka Dar es Salaam huku wakitambua wazi kuwa mkoani kuna mwakilishi wao.

"Ujue mimi nmanilaumu bure kwani mkoa inapotokea ziara ya viongozi wa kitaifa kwanza ofisi za viongozi wenyewe zinapeleka taarifa kwa vyombo mbali mbali vya habari huko huko Dar es Salaam na sisi hapa tunatoa mialiko kwa vyombo vyetu ndani ya mkoa na baadhi ya vyombo ambavyo waandishi wake hawajatoka makao makuu ......nataka ieleweke kuwa hapa pia suala la bajeti linatazamwa hatuwezi kuchukua vyombo vyote zaidi ya 20 katika ziara ya kiongozi wa kitaifa uwezo huo hatuna"

Hivyo alisema lazima vyombo vyenyewe vya habari kupitia wahariri wake kuwa na utamaduni wa kuwatumia waandishi wa mikoani ili kuwafanya nao waweze kushiriki ziara za viongozi hao wa kitaifa katika wilaya za mkoa wao.

Mkuu huyo wa mkoa alisema sababu ya ofisi yake kuendelea kuwatumia waandishi wachache ni kutokana na uwezo mdogo wa kifedha na jinsi ambavyo kwa upande wake anavyoheshimu uwepo wa wanahabari katika mkoa na ndio sababu hata kama baadhi ya wanahabari wanatoka nje ya mkoa ila mkoa umekuwa na kawaida ya kuwachukua wanahabari wachache wa ndani ya mkoa.

Pamoja na kutaja orodha ya waandishi wanne kutoka ndani ya mkoa watakaoshiriki ziara hiyo kesho ambayo haitakuwa na radio hata moja kati ya radio tano zilizopo ndani ya mkoa wala gazeti la Tanzania daima, Mwananchi, Majira , Jambo leo na magazeti mengine maarufu kutokuwepo zaidi ya Dairl news ,gazeti la CCM -Uhuru na The Guardian ila bado mkuu huyo wa mkoa alionekana kuwapoza wanahabari hao baada ya kuahidi kuendelea kutumia zaidi vyombo vya ndani hasa Radio pamoja na magazeti ambayo wahariri wake hawapangi waandishi kutoka Dar es Salaam.

" Ila nataka kusema kuwa kama kuna mwanahabari anataka kugoma ruksa kugoma kwani mtakuwa mnanigomea nini mkuu wa mkoa ama mnaugomea mkoa" alihoji mkuu huyo wa mkoa huku akimtaka mwandishi wa habari hizi ambaye alikuwa aliyekuwa amesimama kupinga kitendo cha baadhi ya vyombo kutengwa kukaa chini na kuwa iwapo wanahabari hao zaidi ya 20 wamefika ofisini kwake kwa lao jambo basi hayupo radhi kuwasikiliza na kutishia kutoka ndani ya ukumbi huo kabla ya wanahabari wa TBC ambao wapo katika orodha wa waandishi wanne kumbembeleza kuendelea na kikao.


"Nasema mimi ndio nimewaita hapa sasa kama wewe Godwin umekuja na hoja yako mimi natoka ...tena nasema kaa chini upesi ..ninyi mmekuja na hoja yenu ya kutaka kugoma basi mimi niondoke kabla ya kuwaeleza nililowaitia hapa leo la ujio wa ziara ya makamu wa rais"

Pia mkuu huyo wa mkoa alitoa sababu ya makamu wa Rais ambaye atakuwepo mkoani Iringa kwa ziara ya siku sita hadi machi 18 mwaka huu kwa kutembelea wilaya ya Njombe ,Ludewa,Kilolo ,Iringa na Mufindi na kuacha wilaya ya Makete kuwa ni kutokana na hali ya hewa mbaya katika mkoa.

Alisema katika ziara hiyo Makamu wa Rais atatembelea miradi mbali mbali ikiwa ni pamoja na kufunguliwa na kuweka mawe ya msingi japo hadi sasa thamani yake haitatolewa kutokana na kubadilika kwa thamani kutokana na siku zinavyo zidi kwenda.

Mwandishi wa mtandao huu alihoji sababu ya mkoa kubagua vyombo vya habari wakati wananchi wakitegemea kupata habari katika vyombo vya ndani ya mkoa kabla ya habari hizo kutoka katika TV na magazeti na kuwa kwa upande wake haungi mkono kubaguliwa kwa Radio za ndani ya mkoa na kutoa nafasi ya vyombo kutoka nje ya mkoa kuja kufanya kazi wakati siku zote katika ziara zake mkuu wa mkoa wanahabari wa ndani ndio wamekuwa wakitumika tena bila malipo kutokana na uzalendo wa mkoa wao na kujua wajibu wao kwa jamii ambayo wanaitumikia.

Kwani alisema ni vigumu kwa wanahabari hao kuingia kila mmoja na usafiri wake wa Tax katika msafara huo hivyo ni vyema mkoa kutoa gari la wanahabari ambalo litakuwepo kisheria tofauti na mwaka jana wakati wa ziara ya rais Jakaya Kikwete ambapo wanahabari walisshushwa katika gari kwa madai kuwa hawakupewa barua za mialiko.


Kwa upande wake katibu mtendaji wa chama cha wanadishi wa habari mkoa wa Iringa (IPC) Frank Leonard alimweleza mkuu huyo wa mkoa kuwa hatua hiyo ya wanahabari kutishia kususia ziara zake imekuja baada ya kuibuka tabia ya ubaguzi ambayo imekuwa ikifanywa na ofisi yake ikiwa ni pamoja na kuchukua chombo kimoja kwa kila ziara iwe ya kitaifa ama mkoa jambo ambalo linajenga makundi miongoni mwa wanahabari.

Leonard alisema katika kuwaunganisha wanahabari wote ni vyema ofisi hiyo ya mkuu wa mkoa ikiwaka utaratibu wa kuwatumia wanahabari wa vyombo vyote bila kujali itkadi ya chombo husika .

Pia alisema kwa kuwa idadi ya wanahabari wanaohitajika katika ziara hiyo ni wanne kutoka ndani ya mkoa bado uongozi wa mkoa unaweza kuwatumia wanahabari zaidi ya 20 katika ziara hiyo kwa kuwapanga kila wilaya wanahabari wanne kama njia ya kujenga umoja kwa wanahabari na ofisi ya mkoa.

Alisema kuwa wananchi wana haki ya kupata habari kutoka katika vyombo hivyo bila kujali itkadi hivyo lazima wakati wa ziara za viongozi wa kitaifa vyombo vyote vipewe mialiko bila kujali posho ambayo si haki ya msingi kwa wanahabari zaidi ya kupata habari.


Wakati huo huo wakazi wa mkoa wa Iringa wameeleza kusikitishwa kwao na hatua ya ofisi ya mkuu wa mkoa kufanya ubaguzi kwa vyombo vya habari na kudai ubaguzi huo umelenga kuficha ukweli wa mambo na kuchagua vyombo vitakavyo pamba ziara zaidi badala ya kueleza mazingira halisi ya kero za wananchi .

Wananchi hao walitoa maoni hayo kwa nyakati tofauti katika kipindi cha Morning Talk cha Radio Ebony FM maarufu mkoani Iringa na mikoa ya nyanja za juu kusini wakati wakijadili habari iliyoandikwa katika gazeti la Tanzania Daima na mtandao wa www.francisgodwin.blogspot.com juu ya wanahabari kupinga ubaguzi wa vyombo vya habari unaofanywa na ofisi ya mkuu wa mkoa wakati wa ziara za viongozi wa kitaifa.

Walisema kuwa wanategemea wanahabri wa ndani ya mkoa kupewa nafasi kubwa katika ziara hiyo kwani ndio ambao wamekuwa wakitumika wakati wote pindi viongozi wa wilaya na mkoa wanapozungukia miradi hiyo.

Usikose kusoma habari hii ndani ya gazeti la Tanzania Daima leo ama usikose uchambuzi maalum kesho kutwa ndani ya gazeti hilo la Taifa Tanzania

Tuesday, March 9, 2010

WANAWAKE MASIKINI MANISPAA YA IRINGA WAPIGWA STOP KUSHIRIKI MAADHIMISHO YA WANAWAKE DUNIANI...............



MAADHIMISHO ya wanawake duniani katika Manispaa ya Iringa yadaiwa kutumika kuwabagua wanawake masikini kwa kuwazuia kuingia ukumbini na kushiriki maandamano kwa kushindwa kulipia kiingilio cha shilingi 2000 ili kushiriki maadhimisho hayo mtandao huu umebaini .


Uchunguzi wa kina uliofanywa na mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com kabla na baada ya maadhimisho hayo jana na leo ambapo mbunge wa jimbo la Iringa mjini Monica Mbega alipata kuwa mgeni rasimi ulibaini sababu ya kuwepo kwa idadi ndogo ya wanawake ni kutokana uongozi wa Mnaispaa ya Iringa chini ya katibu wa sherehe hizo Suzana Nyagawa kuwatoza wanawake shilingi 2000 kila mmoja.


Kutokana kiasi hicho cha fedha kuwa juu ukilinganisha na kipato cha baadhi ya wanawake mjini hapa wengi wao walilazimika kukaa nyumbani huku wachache walieshiriki maandamano hayo kulalamikia hatua hiyo ya kutozwa kiingilio katika sherehe.


Wakizungumza kwa nyakati tofauti na mwandishi wa habari hizi wanawake hao akiwemo akiwemo mjumbe wa kamati kuu ya chama cha NCCR -Mageuzi Taifa Mariam Mwakingwe na mwenyekiti wa umoja wa wanawake wa chama cha mapinduzi (UWT) wilaya ya Iringa mjini Nicolina Lurandara walisema kuwa wanawake wengi walikuwa wakipenda kufika katika maadhimisho hayo ila wameshindwa kufika kutokana na kuchangishwa fedha kwa ajili ya sherehe.


Alisema Mwakingwe kuwa wao kama wanawake wa vyama vya upinzani wamesikitishwa zaidi ya hatua ya uongozi wa manispaa kuwataka wanawake kuchangia sherehe hiyo wakati kimsingi ofisi ya maendeleo ya jamii ambayo sherehe hizo zipo chini yake ilikuwa na uwezo wa kuomba fungu kutoka Manispaa kwa ajili ya sherehe hizo.


Pamoja na kuomba fedha hizo manispaa pia alisema kuna barua zilizosambazwa na kamati ya maandalizi ya sherehe hizo kwa wafanyabiashara na watu mbali mbali kwa ajili ya kufanikisha sherehe hizo hivyo fedha hizo zilikuwa zinatosha kuchangia sherehe hizo kuliko kuwachangisha washiriki.


Hata hivyo alisema utaratibu huu uliotumiwa na Manispaa ya Iringa kuwatoza kiingilio wanawake katika sherehe hizo ni sababu kubwa iliyosababisha wanawake masikini kushindwa kufika katika sherehe hizo na kusikia ujumbe wa maadhimisho hayo.


"Hivi leo hapa anakuja kiongozi wa kitaifa kama Rais Jakaya Kikwete ama waziri mkuu Mizengo Pinda ....wananchi watachangishwa kwa ajili ya kwenda kumsikiliza kiongozi huyo"alihoji na kuwa lazima kamati iliyohusika na sherehe hizo kusoma mapato na matumizi pamoja na kuweka wazi mchango wa halmashauri ya Manispaa ya Iringa na kiasi cha fedha kilichopatikana katika sherehe hizo.


Wakati kwa upande wake mwenyekiti wa UWT Iringa mjini alisema kuwa apingani sana na utaratibu huo wa wananchi kuchangia ila bado ushirikishwaji ulipaswa kuwepo ili kuwasaidia wanawake wenye kipato cha chini nao wapata kushiriki .


Mbunge wa jimbo la Iringa mjini Mbega pia alieleza kusikitishwa kwake na idadi ndogo ya wanawake katika sherehe hizo na kuomba kwa mwakani kutumia CCM kuwavuta wanawake wengi zaidi katika sherehe hizo badala ya kuendelea kuratibiwa na manispaa peke yake.


Wengine walioeleza kusikitishwa kwao na hatua hiyo ya kutozwa kiingilio katika sherehe hizo ni pamoja na mzee Sara Sanga(75) Semeni kalinga (45) na Wende Kyando (50) ambao walisema kwa upande wao walifika katika maandamano hayo bila kujua ila kutokana na kutolipa kiasi hicho cha shilingi 2000 walizuiwa kuingia ukumbini kumsikiliza mgeni rasimi hivyo kulazimika kurudi nyumbani .


" Sisi tulijua kuwa sherehe hii ni kama sherehe nyingine ambazo tumekuwa tukishiriki bila kutozwa kiingilio ....lakini tumekuja kugundua kuwa sivyo baada ya kutakiwa kulipa fedha hiyo kwa madai ya mchango wa kushiriki japo tunajiuliza kuwa hii ni biashara ama ni haki yetu wanawake"


Walihoji wanawake hao huku wakidai kuwa sherehe hizo zimegeuzwa kuwa mradi wa watu wachache ambao umezidi kuwabagua wanawake masikini na kugeuza sherehe hizo kuwa ni sherehe za wanawake matajiri pekee wenye uwezo wa kulipa kiingilio.


Mwandishi wa habari hizi alipomfuata katibu wa sherehe hizo Suzana Nyagawa ambaye ni maratibu wa idara ya maendeleo ya jamii katika Manispaa ya Iringa aligoma kuelezea chochote juu ya suala hilo huku akidai kuwa hayo ni majungu ya wanawake.


"Hawa wanawake hawana dogo yaani yamekuwa hayo tena ....mimi naomba umwone mama Mwalusamba ambae ni mwenyeki wakamati ya sherehe ama mama Mfugale mimi sio msemaji katika hili"


Kwa upande wake mama Mwalusamba aligoma kulitolea ufafanuzi jambo hilo kwa madai hakushiriki kikamilifu katika vikao vya sherehe huku mama Mfugale akieleza kuwa kamati ndio iliyopanga utaratibu huo wa wanawake kuchangia shilingi 2000 kila mmoja kwa ajili ya chakula chao na soda wakati wa sherehe hizo.


Pia alisema suala jingine lililowafanya wanawake kununa zaidi ni lile la vitenge vya sare wakati wa maadhimisho hayo ambavyo vilipelekwa Makete kutokana na ofisi ya manispaa ya Iringa kushindwa kulipia kwa wakati katika ofisi ya mkuu wa mkoa kama ilivyopangwa.


Kuhusu mchango wa Manispaa ya Iringa alisema kuwa Manspaa katika sherehe hizo imechangia gharama za ukumbi,mapambo na muziki katika ukumbi huo.


..............Itaendelea kesho ......................

Friday, March 5, 2010

VIJANA JAZ WAPAMBA SHEREHE ZA KAMANDA WA UV-CCM LUDEWA











Kalenda wa Deo Filikunjombe zagombewa











Mbunge Prof Mwalyosi (kushoto)akiwa na viongozi wa CCM ngazi ya mkoa





Msaada wa gari











Vijana Jaz







SHEREHE za kusimikwa kwa kamanda mpya wa umoja wa vijana wa chama chamapinduzi (UV-CC) mwanahabari na mfanyabiashara Deo Filikunjombe (pichani) zatikisa wilaya ya Ludewa Iringa wana CCM kutoka kata zote 22 za wilaya hiyo washiriki huku wakiwa na fulana zinazosema Tunampenda Deo Filikunjombe washiriki na kumweleza mbunge wao kuwa mapinduzi daima yeye mbunge Prof.Raphael Mwalyosi achanganyikiwa akuna kichwa muda wote.

Akabidhi msaada wa gari la wagonjwa katika kituo cha afya Manda kituo ambacho wagonjwa walikuwa wakipata shida kubwa kutokana na kukosa huduma ya gari la kisasa kwa ajili ya wagonjwa.

Sherehe hizo mbazo ni za kwanza kufanyika kwa bwembwe ikiwa ni pamoja na kushirikisha bendi ya muziki wa dansi ya vijana Jaz Bendi kutoka jijini Dar es Salam kufika kuamba sherehe kama hizo zilizofanyika katika uwanja wa michezo wa mji wa Ludewa sasa na kuhudhuriwa na mgeni rasmi katibu msaidizi wa umoja wa vijana Taifa Mohamed Moyo .

Baadhi ya viongozi wa umoja wa vijana kutoka kata zote za wilaya ya Ludewa ambao walishiriki sherehe hizo wakiongozwa na katibu huyo msaidizi wa umoja huo Taifa na katibu wa UV-CCM mkoa wa Iringa Rhoda George walisema kuwa Filikunjombe ameonyesha mfano mwaka katika kutekeleza ilani ya CCM kwa vitendo ndani ya wilaya hiyo ya Ludewa na mkoa kwa jumla na kuwa wao kama vijana wana muungamkono hata kama ataamua kugombea ubunge katika jimbo hilo katika uchaguzi mkuu utakaofanyika hivi karibuni.

Katibu wa UV CCM wilaya ya Ludewa Meinrard Mtenga katika taarifa yake kwa mgeni rasmi alisema kuwa hata kabla ya kuteuliwa kwake kuwa kamanda wa UV –CCM Filikunjombe amekuwa mstari wa mbele katika kuwatumikia wana Ludewa bila kuwabagua hali ambayo inapelekea umoja huo kuendelea kumuunga mkono kwa nguvu zote.

Alisema Filikunjombe ambaye amepata kuteuliwa kuwa mlezi wa Chipukizi wilaya na Taifa pia ni katibu wa uchumi na fedha wilaya,mjumbe wa kamati ya siasa mkoa wa Iringa na mlezi wa CCM wilaya ya Iringa mjini na mlezi wa chipukizi wa CCM Taifa.

Hivyo alisema kati ya kazi ambazo amepata kufanya ndani ya chama ni pamoja na kutoa msaada wa baiskeli 22 kwa makatibu wa uchumi pia amekuwa mmoja kati ya wafadhili wakubwa walioshiriki kusaidia ujezi wa ofisi ya chama wilaya baada ya kuezuliwa na upepo.

Hata hivyo alisema kazi kubwa ambayo amekuwa akiifanya ni pamoja na kujitolea kusomesha watoto yatima 200 ndani ya wilaya hiyo kwa kuwalipia ada ya sekondari na chuo ,pia kuchangia ujenzi was hue za sekondari ,kusaidia ujenzi wa nyumba za walimu ,pamoja na kusaidia ununuzi wa gari la wagongwa katika kituo cha afya Manda .

Kwa upande wake Filikunjombe amewapongeza wana CCM kwa kujitoeza kwa wingi katika sherehe hizo na kuwa pamoja na baadhi yao kumtaka agombe ubunge ila dabo sherehe hizo ni ushahidi tosha kwake kuwa wananchi wanaunga mkono jitihada zake na wapo tayari kumpa nafasi ya ubunge.

Filikunjombe ambaye pia ni mmoja kati ya wana CCM wanaotaka kugmbea ubunge wa jimbo hilo la Ludewa amepata kuwa mwandishi wa habari wa vyombo mbali mbali hapa nchini vikiwemo vile vya kampuni ya IPP pia amepata kuwa mwandishi wa jeshi la polisi na wizara ya ndani ,BBC na mtaalam wa mawasiliano ya maendeleo katika ofisi ya Rais Ikulu .

Wednesday, March 3, 2010

MASHUJAA WA MKOA WA IRINGA...............














Aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Iringa Bi.Amina Mrisho Said ambaye kwa sasa ni mkuu wa mkoa wa Pwani na mmoja kati ya makada wa CCM anayetaraji kuwania nafasi ya ubunge jimbo la Kiteto akigonganisha grasi na mkuu mpya wa mkoa wa Iringa Bw.Mohamed Abdulaziz ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Lindi mjini ,viongozi hawa walikutana pamoja na juzi katika sherehe ya kumkaribisha mkuu mpya wa mkoa na kumuaga aliyekuwepo pamoja na Ras wake