AMANI YETU TUSIIVURUGE WATANZANIA

AMANI  YETU TUSIIVURUGE  WATANZANIA

POLISI JAMII NA ULINZI SHIRIKISHI AMANI NA UTULIVU VITATAWALA DAIMA TANZANIA

Sunday, April 18, 2010

TIMU YA RADIO EBONY FM YAANZA KUJINOA KUIVAA DSJ...


KIKOSI cha timu ya Radio Ebony Fm Iringa kimeanza maandalizi makubwa ya mchezo wake wa kirafiki kati yake timu ya chuo cha uandishi wa habari Dar es Salaam (DSJ) pamoja na mashindano ya kombe la Mei Mosi mkoani hapa ( pichani ni mchezaji Francis Godwin ambaye ni mmiliki wa mtandao wa www.francisgodwin.blogspot.com)

Msemaji msaidizi wa timu hiyo ya Ebony Fm Bahati Alex alisema kuwa timu hiyo imeanza maandalizi yake mapema ikiwa ni sehemu ya maandalizi yake ya michezo miwili ya kirafiki pamoja na mchezo mmoja wa kuwania kombe la mei mosi mkoa wa Iringa.

Alex alisema kuwa DSJ wapo mbioni kuja mkoani Iringa kwa ziara ya kimasomo na katika ziara yao katika kituo hicho cha Radio pia watapata kuchezo mchezo mmoja wa kirafiki kama njia ya kudumisha mahusiano zaidi .

Hivyo mbali ya kuwapongeza wanafunzi hao wa chuo hicho cha habari kwa kufanya ziara ndani ya mkoa wa Iringa bado alisema uamuzi wao wa kuomba mchezo wa kirafiki ni moja ya changamoto kubwa kwa wadau wa soka ndani ya mkoa katika kufufua soka la Iringa.

Hata hivyo alisema pamoja na mchezo huo kati ya Radio Ebony Fm na DSJ pia alisema mchezo mwingine kama huo wa kirafiki utachezwa mjini Mafinga na timu ya watuma salam mkoa wa Iringa.

Alisema baada ya michezo hiyo miwili kikosi chake kitaendelea na mazoezi ya kawaida kwa ajili ya maandalizi ya kombe la Mei mosi mkoa wa Iringa.

Pamoja kuwataka wadau wa soka ndani ya mkoa kuendelea kuelekeza nguvu zao kwa timu changa ili kama njia ya kuibua vipaji vya wachezaji bado alisema kuwa moja kati ya mikakati ya timu hiyo ni kuendelea kuhamasisha soka zaidi ndani ya mkoa .

Alex alisema kuwa kwa upande wa kikosi chake maandalizi yote yamekamilika kwa ajili ya michezo hiyo miwili ya kirafiki na kuwa hivi sasa kikosi hicho kimekuwa kikijinoa katika uwanja wa chuo cha ualimu Mkwawa mjini hapa.
MWISHO

Saturday, April 10, 2010

KWA HERI BABU MZEE GODWIN SIBONIKE MALILA


Taarifa kwa wadau .Mimi Barack Godwin ni babu yangu kwa niaba ya familia ya mzee Godwin Sibonike Malila wa Soweto Mbeya ninasikitika kutangaza kifo cha baba yangu mdogo mzee Godwin Sibonike Malila (Pichani) kilichotokea tarehe 8 mwezi huu wa nne katika jijini Mbeya.
Habari ziwafikie kaka wa marehemu Bw Kenani Kazimoto Ngao wa Makete Iringa na Ally Kikombe wa Sumbawanga Rukwa Mdogo wa marehemu LUvoneko Siwonike wa Sumbawanga Rukwa na Enock Malila wa Chunya Mbeya.Shemeji wa marehemu Mh.Wiliam Lukuvi mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam na mbunge wa jimbo la Ismani Iringa ,Wadau wenzangu wote katika tasnia hii ya habari pamoja na ndugu jamaa na marafiki popote pale walipo.
Mazishi yanataraji kufanyika leo tarehe 10.4.2010 majira ya saa saba mchana katika makaburi ya sabasaba jijini Mbeya.
Kwa pamoja tunaamini kabisa Mungu ni muweza wa mambo yate pamoja na sisi kumpenda zaidi baba yetu mpendwa Mungu yeye kampenda zaidi yetu hivyo hatuna budi kusema jina la Bwana na libariiwe daima
AMINA
NB. Mpendwa mdau wa mtandao huu kutokana msiba huu napenda kukuomba uvumilivu wako kwa muda wa siku 5 uanzia leo mtandao huu na ule wa http://www.matukiodaima.blogspot.com/ hakuta kuwa na tukio lolote jipya kwani nitakuwepo katika maombolezo .nashukuru kwa ushirikiano wako.Bofya hapa