AMANI YETU TUSIIVURUGE WATANZANIA

AMANI  YETU TUSIIVURUGE  WATANZANIA

POLISI JAMII NA ULINZI SHIRIKISHI AMANI NA UTULIVU VITATAWALA DAIMA TANZANIA

Monday, September 13, 2010

BARABARA YA MAFINGA-KIBAO NI BARABARA MBOVU INYOCHANGIA UCHUMI WA TAIFA


Barabara hii ya Kibao -Mafinga ni barabara inayoiwezesha wilaya ya Mufindi mkoani Iringa kuwa mbele katika makusanyo ya mapato na ni moja kati ya barabara zinazochangia kukuu kwa uchumi wa Taifa la Tanzania kutokana na ukubwa wa kiwanda cha karatasi Mgogolo ambacho ni kiwanda kimojawapo kikubwa kwa Afraka ila barabara yake hadi sasa haina hata chembe ya lami
Hii ni

Friday, September 10, 2010

THOMAS SIMON NYIMBO WA CHADEMA AIWEKA PABAYA CCM NJOMBE MAGHARIBI


Thoma Nyimbo akiwaeleza wananchi wa Ilembula sababu za kugombea kwa Chadema.
Katibu na mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Iringa Bw Alen na Kapwani (kulia) wakisikiliza mabomu ya Nyimbo dhidi ya CCM






Soma hapa

Thursday, September 2, 2010

FARAJA MAFINGA SACCOs YATOA MISAADA KWA YATIMA 300 MUFINDI


Chama cha ushirika cha kuweka na kukopa cha Faraja Mafinga wilaya ya Mufindi mkoani Iringa kimetoa msaada wa mahitaji mbali mbali kwa watoto yatima zaidi ya 300 wanaosoma katika shule za msingi wilayani Mufindi.

Meneja mkuu wa Faraja Mafinga Clever Ndanzi alizitaja a shule zilizonufaika na msaada huo kuwa ni pamoja na shule ya mzingi Upendo ,Mkombwe zote na mjini Mafinga na shule ya msingi Mtula na Matanana wilizopo nje ya mji wa Mafinga na kuwa kila shule watoto yatima 75 watapatiwa msaada huo.

Aliitaja misaada ilitolewa na Chama hicho kwa yatima hao ambao ni msaada uliotokana na sehemu ya faida ya mapato ya mwaka kwa chama hicho ,kuwa ni pamoja na sababuni,mafuta ya kupakaa na vifaa mbali mbali vya shule .

Kwani amesema kuwa chama hicho kimekuwa na utaratibu wa kutumia faida yake inayopatikana kwa mwaka kwa jaili ya kuisaidia jamii yenye shida mbali mbali wakiwemo yatima na watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi pamoja na waathirika wa janga la Ukimwi ndani ya wilaya hiyo.

Ndazi alisema kuwa ushirikia huo ulianzishwa mwaka 1999 na wanachama 18 ambapo hadi sasa kuna jumla ya wanachama zaidi ya 650 ambapo jumla ya mikopo iliyotolewa hadi sasa kwa wanachama wake ni zaidi ya shilingi bilioni 1.

Kwa upande wake mwenyekiti wa ushirika huo Macelina Mosha alisema kuwa pamoja na kuwasaidia watoto hao bado jamii ya wilaya ya Mufindi inanalojukumu la kuendelea kuwasaidia watoto yatima huku akiahidi kuwa chama chake kitaendelea kuwasaidia watoto hao kutokana na faida inayopatikana kila mwaka.

Bi Mosha alisema kuwa mikakati na mwelekeo wa chama hicho unataraji kufahamika wazi siku ya jumamosi wiki hii wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa wanachama ambapo pia wanachama watapokea taarifa ya mwaka ya chama na kujua makisio na mapato na matumizi ya mwaka 2011.
MWISHO